Zoezi la uandikishwaji kwenye daftari la kudumu la kupiga kura kwa njia ya kieletroniki BVR lipo mkoa wa Pwani kwa sasa na linaanza rasmi leo tarehe 7 mwezi wa saba. Zoezi hilo linatarajiwa kumalizika mnamo tarehe 20 ambapo uandikishwa utafanyika kwa awamu na makundi mawili. Mratibu Uchaguzi mkoa wa Pwani ndugu Shangwe Twamala ametoa ufafanuzi wa namna zoezi hilo litakavyofanyika ambapo amesema, awamu ya kwanza itafanyika kwa siku saba kisha baada ya hapo mashine zitahamishwa kwenda sehemu zilizosalia napo zoezi hilo litafanyika kwa siku saba. Pia Shangwe Twamala amewataka wakazi wa Mkoa wa Pwani kujitokeza kwa wingi ili kufaniksha zoezi hilo. FOLLOW INSTAGRAM@sosteneslekule
[via LEKULE]
Follow us @automobileheat – lists / @sectorheat