Quantcast
Channel: AutomobileHeat » electronics
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1695

Maelfu ya wahamiaji waelekea Austria kwa mguu

$
0
0

Maelfu ya wahamiaji waondoka kwa mguu kutoka kituo kikuu cha treni cha Budapest wakielekea kwenye mpaka wa Austria, Septemba 4, 2015 Maelfu ya wahamiaji wameondoka mapema leo Ijumaa alasiri kutoka kituo kikuu cha treni cha Budapest wakijaribu kutembea kwa mguu wakielekea “Austria”, baada ya viongozi wa Hungary kuchukua uamzi Jumanne wiki hii wa kusimamisha usafiri wa kimataifa kwa kutumia reli, ameshuhudia mwandishi wa AFP. Wahamiaji, ambao baadhi yao walikuwa wamekwama katika mji mkuu wa Hungary kwa siku kadhaa, wamesema wanataka kutembea kwa mguu hadi kwenye mpaka wa Austria, ulio kwenye umbali wa kilomita 175, wakati serikali ya Budapest imeongeza jitihada za kuwahamisha kinyume na matakwa yao katika makambi ya mapokezi ya kwanza. Wahamiaji, ikiwa ni pamoja na watoto na watu wanaotumia viti vya magurudumu, wamevuka moja ya daraja kuu katika mji wa Danube bila hofu ya kukamatwa na vikosi vya usalama. Hungary, moja ya nchi kuu wanakopitia wahamiaji kwa kwenda Ulaya ya Kati, kuulionekana wahamiaji wapya 3,300 wakiwasili kwa siku moja pekee ya Alhamisi, shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia wakimbizi limebaini leo Ijumaa. Wakati huo huo Aylan, mtoto mdogo kutoka syria aliyefariki baada ya kuzama katika bahari wakati alipokua akijaribu kukimbia kufuatia mapigano nchini Syria, amezikwa le Ijumaa na familia yake, lakini tukio hilo la kusikitisha ambalo ni ishara kwa mgogoro wa wahamiaji limeendelea kuzua migawanyiko kati ya nchi za Ulaya.

[via LEKULE]

Follow us @automobileheat – lists / @sectorheat


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1695

Trending Articles