Huenda bado haijakufikia taarifa kuhusu ajali ya Askari mmoja ambaye ni msaidizi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Ernest Mangu , kilichonifikia ni taarifa kuhusu mazingira ya tukio la ajali hiyo. Hii ni nukuu ya sentensi ya Kamanda wa Polisi Dodoma > > > ‘ Tulimpata mke wa mkaguzi wa Polisi, Gerard Rioba ambaye ni msaidizi wa IGP , baadae tukampata dereva wa gari lao akiwa amefariki… Tumepata miili ya watoto wake wawili, na baadae tukapata mwili wa marehemu msaidizi wa IGP , Marehemu Rioba ‘- Kamanda David Misime . Marehemu alikuwa na mkewe, watoto wake wawili, msichana msaidizi wa ndani, na msaidizi wake… mazingira ya ajali yanaonesha gari ilisombwa na maji katika eneo la Bwawani, Kongwa Dodoma… #RIP.
[via LEKULE]
Follow us @automobileheat – lists / @sectorheat